Waziri wa Utumishi wa Umma Geoffrey Ruku amewashutumu wakuu katika idara kadhaa za serikali kwa maadili duni ya kazi, akiwataja kama kundi la maafisa wa umma wasio na tija na kuonya kuhusu hatua za haraka dhidi ya mishahara na marupurupu yao

Akizungumza wakati wa mahojiano na kituo kimoja, Ruku alisema serikali imetambua mtindo usio wa kawaida ambapo maafisa wakuu mara kwa mara hukabidhi majukumu kwa wafanyikazi wa chini huku wakitoroka kazini au kuripoti ofisini kwa saa zisizo za kawaida.

Waziri huyo alisema kuwa hali hiyo imedhoofisha utoaji huduma, akibainisha kuwa baadhi ya maafisa wakuu wanakuwa na kiburi baada ya kupanda hadi nyadhifa za juu serikalini.