Mbunge wa Tinderet JuliAs Melly, amewarai wakenya kuendelea kumuunga mkono Rais William Ruto, kuelekea uchaguzi mkuu ujao, akieleza kuwa ana imani na jamii zaidi ya 40 nchini zitapiga kura kumuunga mkono .
Akizungumza katika kaunti ya Nandi kwenye hafla ya kisiasa, Melly ameeleza kuwa Rais atachaguliwa, sio kwa misingi ya kikabila, bali kutokana na utendakazi wake ambao anaamini ni wakupigiwa mfano nchini.

