You are currently viewing LOTEE ATAKA USAWA KATIKA MCHAKATO WA KUTWAA SILAHA HARAMU MIPAKANI

LOTEE ATAKA USAWA KATIKA MCHAKATO WA KUTWAA SILAHA HARAMU MIPAKANI

Mbunge wa Kacheliba, Titus Lotee, ametoa wito kwa serikali kuendesha zoezi la kina la kutwaa  silaha haramu katika maeneo ya rumos na morita,akisema ndo chanzo cha matatizo ya ukosefu wa usalama eneo hilo

Lotee pia ameitaka serikali kuwatuma  maafisa wa   KPR , katika maeneo hayo ili kushirikiana na wale wa KDF  kuimarisha usalama na kulinda maisha na mali ya wananchi.

Ameonya kuwa kushindwa kuchukua hatua za haraka kunaweza kuwalazimu baadhi ya wakazi kuanza kuchukua sheria mikononi , akiweka bayana haja ya usawa katika mchakato wa kutwaa silaha haramu mikononi mwa raia  ili kurejesha usalama 

APERIT FM,HII NI YETU