Washukiwa tisa wa uhalifu wamekamatwa katika kaunti ya Trans Nzoia.

Kulingana na idara ya Upelelezi wa makosa ya Jinai (DCI), washukiwa hao walinaswa wakati wa operesheni iliyoongozwa na ujasusi iliyolenga wahalifu katika Kaunti Ndogo ya Trans Nzoia Magharibi.

Operesheni hiyo iliendeshwa kwa pamoja na maafisa kutoka Makao Makuu ya DCI na Kituo cha Polisi cha Kitale.

Polisi walisema operesheni hiyo ililenga maeneo ya Premium na Tuwani, ambayo ni maeneo yanayokumbwa na ghasia za magenge hivi karibuni.

“Kwa kutumia taarifa za kijasusi za kuaminika, timu hiyo iliwakamata upesi washukiwa hao, na kusambaratisha kundi ambalo limekuwa likiwatisha wakazi na kuvuruga utulivu wa umma,” polisi walisema.

Washukiwa hao kwa sasa wako rumande, huku wakisubiri kufikishwa mahakamani.