You are currently viewing GAVANA ROTICH AKARIRI HAJA YA KUENDELEA KUTWALIWA BUNDUKI HARAMU NA AMANI KUDUMISHWA NCHINI

GAVANA ROTICH AKARIRI HAJA YA KUENDELEA KUTWALIWA BUNDUKI HARAMU NA AMANI KUDUMISHWA NCHINI

Gavana wa kaunti ya  Egeyo Marakwet, Wisley Rotich,ameitolea mwito wizara ya usalama kuendeleza mchakato wa kuhakikisha silaha zote haramu zilizo mikononi mwa raia zinarejeshwa ili kushuhudiwa amani ya kudumu

Akizungumza katika eneo la Kamoi Marakwet Magharibi Gavana Rotich amesema utwaaji wa silaha hizo kutasaidia kuhakikisha maendeleo inafika mashinani kwa faida ya wananchi

Aidha ameonya kuhusu kauli za viongozi kwenye majukwaa tofauti ya kisiasa akisema huenda zikachangia kugawanya   taifa kwa misingi mbalimbali

Amemsuta aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua, kutokana na kauli zake za  kuchochea umma kwa misingi ya kikabila,akisema viongozi wanapaswa kuelekeza nguvu zao katika masuala ya maendeleo na changamoto zinazowakabili wananchi, badala ya kujihusisha na kauli zinazochochea mijadala ya kisiasa.

APERIT FM ,HII NI YETU