You are currently viewing UHISPANIA YAONGOZA VIWANGO VYA FIFA

UHISPANIA YAONGOZA VIWANGO VYA FIFA

Uhispania kileleni kwenye viwango vya FIFA baada ya kutwaa Kombe la Dunia. Mexico, Norway na Marekani zikipanda kwa kasi kubwa.

Uhispania imepanda hadi nafasi ya kwanza kwenye viwango vya FIFA baada ya kuishinda Argentina 1–0 katika fainali ya Kombe la Dunia.

Argentina, iliyokuwa ikiongoza viwango hivyo, sasa imeshuka hadi nafasi ya pili. Ufaransa na England zimeendelea kushikilia nafasi ya tatu na nne licha ya England kuishinda Ufaransa katika mechi ya mshindi wa tatu.

Brazil na Morocco wameipita Ureno katika nafasi ya tano na sita, wakati Mexico ikipanda hadi nafasi ya 10 kufuatia kampeni nzuri kwenye Kombe la Dunia. Marekani imepanda hadi nafasi ya 16, huku Norway ikiwa miongoni mwa timu zilizopanda zaidi, ikifikia nafasi ya 19 baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika Kombe la Dunia.

Kwa upande mwingine, Tunisia imeshuka kwa nafasi 12 hadi nafasi ya 57 baada ya kushindwa kufuzu hatua ya mtoano. Ujerumani ipo nafasi ya 12, huku Japan ikiwa ya 17 na Senegal nafasi ya 18.