You are currently viewing KUSHINDWA KWA KENYA KWANZA OLKALAU HAIDHIHIRISHI KUPOTEZA KWENYE UCHAGUZI UJAO

KUSHINDWA KWA KENYA KWANZA OLKALAU HAIDHIHIRISHI KUPOTEZA KWENYE UCHAGUZI UJAO

Mwakilishi wa akina mama  kaunti ya Pokot  Magharibi   Rael Kasiwai Aleutum, amesema kuwa kushindwa kwa  kenya kwanza katika uchaguzi mdogo wa Ol Kalou ni tukio ambalo halipaswi kutafsiriwa kama mwelekeo wa siasa za uchaguzi mkuu ujao.

Kulingana na Kasiwai   serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo na kushughulikia mahitaji ya wananchi ili kuimarisha imani yao.


‎Aidha, ametangaza kuwa ana imani Rais William  Ruto atahudumu kwa mihula miwili kamili, akisema viongozi wa muungano huo wataendelea kufanya kazi kwa pamoja kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.