Vijana kutoka eneo bunge la Cherang’any wameanzisha vuguvugu la kuhamasisha uwezeshaji wa kiuchumi na kudumisha amani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka ujao
Kampeni hiyo inalenga kuwahimiza vijana kujihusisha na shughuli za kujikwamua kiuchumi, huku wakijiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani kama ukabila, uhalifu, matumizi ya dawa za kulevya na vurugu za kisiasa.
Viongozi wa vuguvugu hilo wamesema mshikamano wa jamii ni muhimu katika kipindi hiki cha uchaguzi, ili kuhakikisha mchakato huo unafanyika kwa utulivu na bila migawanyiko.

