You are currently viewing GAVANA ROTICH AWAONYA WAKAZI DHIDI YA POMBE KABLA YA MVUA KUBWA

GAVANA ROTICH AWAONYA WAKAZI DHIDI YA POMBE KABLA YA MVUA KUBWA

Gavana wa  kaunti ya  Elgeyo Marakwet, Wisley Rotich, amewataka wakazi kuchukua tahadhari kufuatia utabiri wa  mvua za El Niño ambao unatarajiwa kusababisha  changamoto katika maeneo mbalimbali ya kaunti hiyo.

‎Aidha, gavana Rotich amesema serikali ya kaunti inapanga kuwahamisha kwa lazima wakazi wanaoishi katika maeneo yaliyo katika hatari ya maporomoko ya ardhi.

Amesema hatua hiyo inalenga kuzuia maafa mengine kama yaliyoshuhudiwa katika eneo la Chesongoch, huku serikali ikisisitiza umuhimu wa wakazi kushirikiana na mamlaka wakati wa utekelezaji wa hatua za usalama.

Rotich amewataka wananchi kuwa waangalifu, kufuatilia taarifa za hali ya hewa na kuzingatia maagizo ya serikali ili kulinda maisha na mali zao wakati wa msimu wa mvua.

Aidha amewataka  wenyeji kutumia kipindi hicho cha mvua kuzalisha vyakula ili kuondokana na njaa hasa baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kilichosababisha hasara msimu huu

APERIT FM,HII NI YETU