You are currently viewing BARAZA LA WAZEE WA JAMII YA POKOT LASHTUMU UVAMIZI ULIOTOKEA KATIKA ENEO LA OMBOLION

BARAZA LA WAZEE WA JAMII YA POKOT LASHTUMU UVAMIZI ULIOTOKEA KATIKA ENEO LA OMBOLION

Baraza la wazee wa jamii ya Pokot limeelezea kutamaushwa na kisa cha uvamizi na wizi wa mifugo  katika eneo la Ombolion Pokot Kaskazini, swala wanalodai linachangiwa na kuwepo kwa silaha haramu miongoni mwa wakaazi wa kaunti jirani ya turkana.

Baraza hilo likiongozwa na  Mastait Lokiles linasema  silaha haramu zilizoko mikononi mwa raia katika  kaunti jirani ya Turkana imepelekea kuzuka tena uvamizi huo licha ya idara ya usalama na viongozi kushinikiza usalimishaji wa silaha hizo kaskazini mwa bonde la ufa.

 Anasema   baraza la wazee wa jamii ya Pokot wanaunga mkono oparesheni ya serikali kutwaa bunduki   japo mpango huo unapaswa kutekelezwa kwa usawa katika kaunti zote zinazoshuhudia uhalifu.