Waziri wa usalama Kipchumba Murkomen, ameendelea kukosolewa vikali kufuatia matukio ya uhalifu yanayohusisha wizi wa mifugo na machafuko kwenye kaunti za bonde la Kerio na maeneo mengine nchini na hatua zinazochukuliwa kushughulikia tatizo hilo
Kulingana na seneta wa Nandi Samson Cherargei inashangaza kwamba washukiwa wanaodaiwa kuhusika na kifo cha padre marehemu Allois Bett bado hawajakamatwa, licha ya serikali kutoa hakikisho mara kadhaa kwamba hatua zitachukuliwa dhidi yao.
Aidha amehoji matumizi ya mamilioni ya fedha katika vikao vya jukwaa la usalama, licha ya visa vya ukosefu wa usalama kuendelea kushuhudiwa katika kaunti ya Turkana na pokot magharibi huku pia akipendekeza kuanzishwa kwa hazina maalum ya fidia kwa waathiriwa wa visa hivyo
Cherargei ametaka serikali kutoa maelezo kuhusu matokeo ya vikao hivyo na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha usalama wa wananchi unaboreshwa.
APERIT FM,HII NI YETU

