You are currently viewing VIONGOZI WA KISIASA KAUNTI YA TRANS-NZOIA WATAKIWA KUWEKEZA KATIKA MIRADI YA KUWAWEZESHA VIJANA BADALA YA KUWATUMIA VISIVYO

VIONGOZI WA KISIASA KAUNTI YA TRANS-NZOIA WATAKIWA KUWEKEZA KATIKA MIRADI YA KUWAWEZESHA VIJANA BADALA YA KUWATUMIA VISIVYO

Seneta wa Trans -Nzoia, Allan Chesang, amewataka viongozi wa kisiasa kuacha kuwatumia vijana kutekeleza vitendo vya vurugu na uhalifu wa kisiasa kwa manufaa yao.


‎Chesang amesema badala ya kuwahusisha vijana katika machafuko, viongozi wanapaswa kutumia rasilimali walizonazo kuwawezesha kupitia fursa za elimu, ajira, biashara na ujasiriamali ili kuboresha maisha yao.


‎Amesisitiza kuwa kuwawezesha vijana kiuchumi kutawapa matumaini ya maisha bora, kupunguza ushawishi wa kujiingiza katika vitendo vya kihalifu na kuchangia kudumisha amani, umoja na maendeleo ya nchi