Mbunge wa Tiaty, William Kamket, amependekeza mfumo wa demokrasia ya maafikiano kati ya maeneo ya tiaty na baringo kaskazini kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.
Kamket amesema Tiaty iko tayari kumuunga mkono mgombea wa ugavana kutoka Baringo Kaskazini huku akipendekeza kuwa eneo hilo limuunge mkono mgombea kutoka tiaty katika nafasi ya uwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Baringo.
Kwa mujibu wa Kamket, mpango huo unalenga kuimarisha ushirikiano wa kisiasa, kudumisha umoja, na kupunguza ushindani unaoweza kugawanya viongozi na wananchi wa kaunti hiyo kabla ya uchaguzi wa mwaka 2027.

