Waziri wa elimu, Migos Ogamba, amesema mfumo mpya unaopendekezwa wa ufadhili wa elimu ya juu utaanza kutekelezwa baada ya kuidhinishwa na bunge.
Ogamba amesema wanafunzi watakaojiunga na vyuo vikuu na vyuo vingine vya elimu ya juu mwezi septemba wataandikishwa chini ya mfumo wa sasa
Ameongeza kuwa wanafunzi hao watahamia katika mfumo mpya baada ya mswada uliowasilishwa bungeni kupitishwa na kuwa sheria.
Kulingana naye mageuzi hayo yanalenga kubadilisha mfumo wa serikali wa kuzingatia kipato cha familia, na badala yake kuelekeza uwekezaji moja kwa moja kwa wanafunzi na mustakabali wao.

