Mbunge wa Turkana Kusini, John Ariko Namoit, ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka kulinda sekta ya boda-boda dhidi ya kampuni za mikopo anazodai zinawanyanyasa wanabodaboda
Dkt. Namoit amesema baadhi ya kampuni za utoaji mikopo zimekuwa zikiweka waendesha boda-boda katika hali ngumu kwa kuwapa mikopo ya kununua pikipiki, lakini baadaye kuwanyang’anya pikipiki hizo wanaposhindwa kukamilisha malipo yao
Ariko amesema hali hiyo inawaweka wahudumu hao katika mazingira magumu ikizingatiwa pikipiki ndiyo chanzo chao kikuu cha mapato
ameitaka serikali kuchukua hatua kuhakikisha kuwa kampuni zinazotoa mikopo kwa waendesha boda-boda zinafanya shughuli zao kwa uwazi, bila kuwanyonya wananchi wanaotegemea mikopo hiyo kujiajiri.
APERIT FM,HII NI YETU

